Trump Awaonya Washirika wa Kibiashara wa Iran

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Trump Awaonya Washirika wa Kibiashara wa Iran
Rais wa Marekani Donald Trump ametoa onyo kali kwa mtu yeyote anayeshirikiana kibiashara na Iran kufuatia hatua yake ya kuiwekea vikwazo nchi hiyo.

''Yeyote atakayefanya biashara na Iran hataruhusiwa kufanya biashara na Marekani'' , rais huyo alituma ujumbe wa twitter.

Vikwazo vikali vilianza kutekelezwa usiku wa kuamkia leo na vingine vikali vinavyohusiana na mafuta vitaanza mwezi Novemba.

Rais wa Iran amesema kuwa hatua hizo ni vita vya kiakili ambavyo vinalenga kuleta mgawanyiko miongoni mwa raia wa Iran.

Vikwazo hivyo vinafuatia hatua ya Marekani kujiondoa katika makubaliano ya kinyuklia ya Iran mapema mwaka huu.

Makubaliano hayo , yalioafikiwa wakati wa utawala wa rais Barrack Obama ,yaliilazimu Iran kusitisha mpango wake wa kinyuklia huku vikwazo dhidi yake vikiondolewa.

Rais Trump ameyataja makubaliano hayo 'yanayopendelea upande mmoja'' kuwa mabaya zaidi kuwahi kufanyika.

Anaamini kwamba shinikizo mpya za kiuchumi zitailazimu Iran kuingia katika makubaliano mapya.

Muungano wa Ulaya, ambao bado unaunga mkono makubaliano hayo ya Iran , umezungumza dhidi ya vikwazo hivyo ukiapa kulinda kampuni zinazofanya biashara halali na Iran.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad