AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza leo Septemba 25, 2018 wakati wa uzinduzi huo, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema sera hizo zitakuwa zinafanyiwa marekebisho kulingana na wakati.
Amesema eneo la kwanza lililoko kwenye sera hiyo ni ile inayolinda uhuru wa wananchi.
Mbowe amesema Mwalimu Julius Nyerere aliwahi kuzungumzia suala la maendeleo ya watu na uhuru, jambo ambalo wamelijadili kwa kina kwenye sera hiyo.
Amelitaja eneo lingine ni nafasi kuwa na sera zinazolenga misingi ya uchumi.
Amesema katika eneo hilo wameainisha ni kwa namna gani wananchi watapata huduma za kijamii.
Amefafanua eneo hilo limeainisha namna uchumi utakavyokuwa endelevu badala ya kuwa uliohodhiwa na Serikali.
Mbowe ameitaja sera nyingine ni zinazoilinda na kuihuisha jamii kupata huduma ya maji, barabara yasiwe mambo yanayofanywa na sekta binafsi bali yafanywe na Serikali.
"Sasa hivi kumejengeka dhana kuwa Serikali uliyojenga shule, zahanati inakuwa ni kama msaada, hii si sawa hayo ni majukumu ya Serikali," amesema Mbowe.
Mbowe amesema kabla ya kutayarisha sera hiyo wametumia mwaka mzima kufanya tafiti na kukusanya maoni kutoka kwa watu mbalimbali.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK