AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akionesha kukasirishwa na ukatili huo Baba mzazi wa mtoto huyo Ali Khamis Mbarouk maarufu Ali Gaga mkazi wa Koani amesema kitendo hicho kimefanyika mtaa wa Kwahani wilaya ya Mjini Unguja ambapo Mama mzazi na Bibi walimchoma moto wa makaratasi kwenye vidole vya mikono ya mtoto huyo na hadi sasa hali yake sio nzuri.
Amesema baada ya kufanya kitendo hicho mama mzazi wa mtoto ambaye alikuwa mke wake alimpigia simu majira ya usiku baada ya kuona hali ya mtoto sio nzuri kutokana na kulia sana hali iliyopelekea kupatwa na homa.
“Asubuhi nilikwenda kumuona mtoto wangu na kumkuta katika hali mbaya anaumwa na hawezi kushika kitu chochote hivyo nikampeleka hospitali na madaktari baada ya kuona hali ya mtoto walilaani kwani adhabu zipo nyingi kwanini wamchome moto” Amesema baba mzazi wa mtoto.
Nae Sheha wa shehiya ya Kwahani Machano Mwadini Omar amelaani kitendo hicho na kusema si kitendo kizuri wao kama wazazi kumtendea mtoto wao hivyo ameviomba vyombo vya sheria vichukuwe hatua iwe fundisho ili tukio kama hilo lisije kujirejea.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK