Mama Amchoma Moto Mwanae Akimtuhumu Kuiba Laki 2

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mama Amchoma Moto Mwanae Akimtuhumu Kuiba Laki 2
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni Muliro Jumanne Muliro amethibitisha kukamatwa kwa mwanamke anayetuhumiwa kumuunguza mtoto wake wa kumzaa kwa mafuta ya taa kwa madai ya kuiba kiasi cha shilingi laki mbili zilizokuwa zimehifadhiwa ndani.

 Kamanda Muliro amesema mtoto aliyefanyiwa ukatili huo ni wa kike ambaye anasoma kidato cha kwanza shule ya Sekondari Magomeni na alifanyiwa hivyo usiku wa kuamkia Septemba 1, 2018 maeneo ya Boko Magereza.

''Hili ni kosa la jinai na alikusudia huwezi kusema ni bahati mbaya wakati mtu amenunua mafuta na amefanya maandalizi kabisa, kwahiyo sisi kama chombo cha dola kazi yetu ni kuhakikisha tunamfikisha katika mkono wa sheria kwa ukatili aliomfanyia mtoto wake mwenyewe'', amesema.

Kamanda Muliro ameweka wazi kuwa mtuhumiwa atafikishwa mahakamani muda wowote kuanzia sasa kwakua taratibu za kipolisi zimekamilika.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad