Mtalii wa Kwanza Atakayekwenda Kwenye Mwezi Atangazwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mtalii wa Kwanza Atakayekwenda Kwenye Mwezi Atangazwa
Kampuni ya tajiri maarufu Elon Musk ya SpaceX imetangaza nani atakuwa abiria wake wa kwanza, mtalii, ambaye atasafirishwa kwenda kuuzunguka Mwezi.

Mtalii huyo atakuwa ni bilionea Mjapani Yusaku Maezawa, 42, ambaye pia ni mjasiriamali na mwenye biashara kubwa ya uuzaji wa mitindo ya mavazi na ubunifu kupitia mtandao.

Mwenyewe ametangaza: "Nimeamua kwenda kwa Mwezi."

Anatarajiwa kusafiri kwa kutumia chombo cha roketi kwa jina Big Falcon Rocket (BFR), ambacho ni chombo cha usafiri wa anga za juu kilichozinduliwa na Bw Musk mwaka 2016.

Hiyo itakuwa mara ya kwanza kwa binadamu kwenda kwenye Mwezi tangu safari zilizofanywa na wana anga walioabiri chombo cha Apollo 17 cha Shirika la Anga za Juu la Marekani (Nasa) mwaka 1972.

Tangazo kwamba Yusaku atakuwa wa kwanza kufanya ziara hiyo ya kihistoria lilifanywa katika makao makuu ya SpaceX mjini Hawthorne, California, siku ya Jumanne.

Kampuni hiyo imesema safari hiyo itakuwa "hatua kubwa sana katika kuwezesha watu wa kawaida ambao wamekuwa na ndoto ya kusafiri anga za juu wakati mmoja maishani".

Awali kwenye Twitter, Bw Musk alikuwa tayari amedokeza kwamba abiria huyo atakuwa kutoka Japan.

Ni wanadamu 24 pekee ambao wamewahi kusafiri kwenda kwenye Mwezi na wote walikuwa Wamarekani.

Hii ni kutokana na hali kwamba itategemea chombo cha anga za juu ambacho bado hakijaundwa kufikia sasa.

Mwaka 2017, Musk alitangaza kwamba atakuwa akiwatuma watalii wawili, ambao watalipia gharama ya safari hiyo, kwenda kuuzunguka Mwezi.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad