Updates: Miili Mingine Mitano Yaopolewa Ajali MV Nyerere.....Waliofariki Dunia Wafika 157

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Updates: Miili Mingine Mitano Yaopolewa Ajali MV Nyerere.....Waliofariki Dunia Wafika 157
Idadi ya watu waliofariki dunia katika ajali ya kivuko cha MV Nyerere kilichozama juzi mchana Septemba 20, 2018 imefikia 157  huku uokoaji ukiendelea.

Akizungumza akiwa katika eneo la tukio, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella amesema miili mingine imeopolewa leo asubuhi Septemba 22, 2018.

“Leo miili mingine imeopolewa lakini bado uopoaji unaendelea,” amesema.

Amesema vikosi vya uokoaji vinaendelea na shughuli ya uokoaji na ikitarajiwa shughuli hiyo kufanyika hadi kesho Jumapili.

“Vikosi vya uokoaji vinafanya kazi yake vizuri na tunaendelea na tunatarajia Mungu akijalia hadi kesho tutakuwa tumekamilisha,” alibainisha mkuu huyo wa mkoa.

Mongella amesema kuwa baadhi ya miili imeshatambuliwa huku kazi ya utambuzi akisema inaendelea.

“Hadi jana (Ijumaa Septemba 21, 2018) miili 116 imeshapata ndugu na tunaamini miili mingine itatambulika maana wananchi wanaendelea kuwasili kuja kuitambua,” amesema Mongella.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad