AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kwa mujibu Waziri Mwalimu usambazaji wa picha hizo zinaongeza majonzi kwa ndugu na waathirika wa tukio la ajali ya Mv-Nyerere badala yake amewataka watanzania kutumia nafasi hiyo kuwaombea.
Ummy Mwalimu ameeleza hayo kupitia ukurasa wa Twitter.
"Ndugu zangu Watanzania, ninawaomba sana TUACHE KUSAMBAZA NA KUPOSTI PICHA ZA MAREHEMU WA AJALI YA MV NYERERE.
"Tuheshimu Utu na Ubinadamu wao. Lakini pia watu wapo kwenye majonzi makubwa ya kupoteza wapendwa wao, hivi kuna faida gani kwa baadhi yetu sisi kuposti picha hizi za marehemu?.
"Tafadhali tuwapunguzie maumivu familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu kwa kuto-posti picha hizi. Muhimu tuendelee kuwaombea familia za marehemu Mwenyezi Mungu awape subra na ustahamilivu ktk kipindi hiki kigumu. Aidha tuwaombee rehema wenzetu waliotangulia mbele ya haki. #MbeleYaoNyumaYetu "
aliimalizia Waziri Mwalimu.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK