AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Sakaya amesema kuwa kikao hicho kitatoa majibu endapo wataendelea au watajiondoa kwa yale yanayojitokeza kwenye chaguzi zilizopita ikiwemo mawakala wake kutopewa fomu za kusimamia kura katika baadhi ya vituo.
Sakaya amefunguka hayo katika mahojiano na www.eatv.tv, ambapo amesema kuwa uchaguzi uliopita katika jimbo la Liwale CUF walionewa na kuporwa jimbo hilo ambalo lilikuwa ni ngome yao.
"Nilikuwepo Liwale nmeshuhudia kila kitu, CCM wametuibia kura zetu kwani asilimia 75 ya wapiga kura waliipigia kura CUF lakini mawakala wetu walinyimwa fursa ya kusimamia na kuhesabu kura zetu", amesema Sakaya.
Marudio ya uchaguzi wa jimbo la Liwale yalifanyika, Oktoba 13, baada ya aliyekuwa mbunge wake Zuberi Kachauka (CUF) kujiuzulu na kujivua uanachama na kujiunga na chama cha mapinduzi (CCM), ambapo aliteuliwa kuwa mgombea kupitia chama hicho na baadae kuibuka mshindi katika uchaguzi huo wa marudio.
CHADEMA kupitia mwenyekiti wake wa chama, Freeman Mbowe kilitangaza kujiondoa rasmi kushiriki chaguzi ndogo zote zilizotangazwa kufanyika hivi karibuni na chaguzi zozote zitakazofuata zinazosimamiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwa madai kwamba tume hiyo inafanya kazi kwa niaba ya Chama Cha Mapinduzi.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK