Ndalichako aingilia kati wanafunzi 682 waliofutiwa usajili UDSM

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Ndalichako aingilia kati wanafunzi 682 waliofutiwa usajili UDSM
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako, ameagiza wanafunzi 682 walioondolewa katika usajili wa chuo Kikuu cha Dar es Salaam kurudishwa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Jumatatu Oktoba 22, muda mfupi baada kufungua mafunzo ya wahasibu yanayoendelea jijini Dar es Salaam Profesa Ndalichako amesema amesikia suala hilo mwishoni mwa wiki na tayari ameshauagiza uongozi wa Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) na uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kukaa pamoja na kumaliza tofauti hizo.

“Chuo Kikuu kina nafasi 3,000 tatizo lilikuwa ni la kiufundi kutokana na wanafunzi wengi kupenda chuo hicho ,hivyo nimeomba uongozi kumaliza tatizo hilo na watoto waweze kupokelewa.

“Wengi wanapenda UDSM na tatizo lilikuwa linaweza kurekebishika na wote ni idara za serikali, TCU na UDSM hawakutakiwa kushindana na ndiyo maana nimewaagiza hadi Jumamosi wawe wamemaliza tofauti zao nafikiri hadi leo saa tisa watakuwa wameshawekana sawa,” amesema Profesa Ndalichako.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad