TCU Yaongeza Kwa Mara Nyingine Kwa Wanaoomba Vyuo Vikuu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

TCU Yaongeza Kwa Mara Nyingine Kwa Wanaoomba Vyuo Vikuu
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), imefungua dirisha la udahili kwa mara ya nne kwa waombaji ambao hawakuchaguliwa katika awamu zilizopita.

Kwa mujibu wa taarifa iliyowekwa kwenye tovuti ya TCU, iliyotolewa na Katibu Mtendaji, ilieleza kuwa udahili huo ni kwa wanafunzi wanaotaka kujiunga na vyuo vikuu kwa mwaka wa masomo 2018/19.

Aidha, taarifa hiyo ilieleza kuwa udahili ulianza Oktoba 13 na utaendelea hadi 20, mwaka huu.

“Waombaji wapya na wale ambao hawakuchaguliwa katika awamu zilizopita wanahimizwa kutumia fursa hii ya mwisho kutuma maombi yao ya udahili moja kwa moja kwenye vyuo na taasisi za elimu ya juu nchini,” ilifafanua taarifa hiyo.

Aidha, taarifa hiyo ilibainisha kuwa waombaji wote wanakumbushwa kuomba programu ambazo wanakidhi vigezo kama ilivyoelekezwa katika kitabu cha mwongozo wa udahili na kwamba tume inaelekeza vyuo na taasisi za elimu ya juu kutangaza programu ambazo bado zina nafasi na idadi ya nafasi zilizobaki ili waombaji waweze kutuma maombi yao.

Hivi karibuni, TCU iliwataka waombaji wote wa vyuo waliochaguliwa kwenye chuo zaidi ya kimoja, kuthibitisha udahili wao na mwisho ilikuwa Oktoba 5, mwaka huu.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad