AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Magufuli ameelekeza hivyo leo alipokutana na viongozi wa Shirikisho la Wafanyakazi (TUCTA), vyama shiriki, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (PSSSF & NSSF) na Mamlaka ya Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii (SSRA), Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Pamoja na uamuzihuo, rais pia alizitaka hifadhi za jamii zipunguze matumizi ya hovyo, ili kuweza kuwalipa wanachama wake vizuri na mapema.
“Tunahitaji watu wetu wapate fedha nyingi walipwe, lakini pia tunahitaji huu mfuko usife, hii ‘formula’ haipo duniani, mtu anamaliza halafu kiwango chake unakizidisha mara nne, hii haipo,” alisema rais na kutolea mfano mawaziri na wabunge ambao hulipewa mafao yao yote na kwa wakati mmoja.
Akifafanua, alisema kwamba wakati anashika madaraka kulikuwa na deni la Sh. trilioni 1.2 katika mifuko hiyo na hivyo ilikuwa ni shida kuwalipa.
“Tulipongia madarakani tulikuta deni la trilioni 1.2, serikali yenyewe haijachangia hii mifuko, waliostaafu kwa wakati ule ilikuwa ni shida, kwani hata ile michango ya serikali haitekelezwi,” alisema na kuongeza kwamba mifuko mingine ilikuwa ikiendeshwa kiajabu ikiwa ni pamoja na kuanzishwa miradi ya kiajabu… na miradi mingi ilikuwa ya majengo.
Aliongeza kwamba mifuko ya jamii yote ilikuwa na hali mbaya, kwa sababu haikuwa imeratibiwa vyema ambapo “waendesha mifuko wote walikuwa wanapigana vita, wanagombania wanachama, walikuwa hawapendani…”
Alisema serikali iliamua kuunganisha mifuko hiyo ikiwa ni pamoja na makubaliano kwamba NSSF ifanyiwe marekebisho, hatua iliyotokana na ombi la muda mrefu la vyama vya wafanyakazi waliotaka kuunganishwa kwa mifuko hiyo.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK