''Yanga na Azam FC Wanapanga Matokeo''- Haji Manara

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Katika kipindi cha miaka kadhaa ambayo Simba haikushiriki michuano ya kimataifa, msemaji wake Haji Manara alikuwa akipambana na Bodi ya ligi (TPLB) juu ya Yanga na Azam FC kuwa na viporo vingi na kufikia hatua ya kusema wanapanga matokeo.


Hivi sasa mambo yamegeuka na huenda Haji Manara anatamani maneno haya, ''Kama ambavyo Yanga na Azam FC wanapanga matokeo'', yafutike lakini teknolojia imetunza na yanatumika kama kumbukumbu ikimkumbusha kuwa mambo yamegeukia kwake wakati huu ambao Simba ina viporo 7 vya ligi kuu soka Tanzania bara.

Akiwa kwenye moja ya mikutano ya klabu na wanahabari miaka iliyopita Manara alisema, ''Kwa kawaida timu inatakiwa kucheza mechi moja na kupumzika ndani ya saa 72 lakini Bodi ya ligi inatoa maelezo mengi kitu ambacho si sawa''.

Aidha Manara aliweka wazi kuwa Yanga ambayo ilikuwa na viporo 9 ilikuwa inapanga matokeo kwa kutumia mfumo wa 'Indirect' kwani kuna baadhi ya timu ambazo zilikuwa zinakaribia kushuka daraja huenda zisingekuwa na ushindani wakati ambao zitacheza na Yanga.

Hata hivyo kwa upande wa pili ambao ni Yanga na Azam FC msimu huu wao wapo kimya na hawajalalamika licha ya Simba kupumzika kwa zaidi ya saa 72 lakini imekuwa haichezi mechi zake za ligi na kuendelea na maandalizi ya michuano ya kimataifa.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad