Azam FC yakabwa koo na Ruvu Shooting

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Timu ya Ruvu Shooting ya Pwani imetoa sare ya bila kufungana na Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani.

Kwa matokeo hayo Azam FC inafikisha pointi 41 baada ya kucheza mechi 18, ikiendelea kushika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu, nyuma ya Yanga SC yenye pointi 53 za mechi 19 na mbele ya mabingwa watetezi, Simba SC wenye pointi 33 za mechi 14.

Ruvu Shooting inafikisha pointi 24 baada ya kucheza mechi 22 na kupanda kwa nafasi moja tu kutoka ya 14, sasa ikiwa mbele ya Stand United ya Shinyanga yenye pointi 23 za mechi 22.

Mechi nyingine za Ligi Kuu leo, Mbao FC imeweza kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Singida United kwenye Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza.

Nayo Biashara United imeendelea kufanya vyema chini ya kocha mpya, Amri Said ‘Stam’ baada ya kuibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Stand United.

African Lyon imepata ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Kagera Sugar Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam.

Nayo Ndanda FC imeutumia vyema Uwanja wa nyumbani, Nangwanda Sijaona, Mtwara baada ya kuibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya JKT Tanzania
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad