Mc Pilipili Afunguka Sababu ya Kumwaga Chozi Wakati wa Kumvalisha Pete Mchumba Wake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mc Pilipili Afunguka Sababu ya Kumwaga Chozi Wakati wa Kumvalisha Pete Mchumba Wake
Baada ya hivi karibuni mchekeshaji maarufu Bongo, Emmanuel Mathias ‘MC Pilipili’ kumvisha pete ya uchumba, mchumba’ke, Philomena Thadei na kuangua kilio, mwenyewe ameibuka na kufichua kilichomliza.



MC Pilipili aliangua kilio cha aina yake wakati akimvisha pete mrembo huyo na kuzua gumzo la aina yake kwani imezoeleka kwenye zoezi kama hilo mara nyingi wanawake ndiyo huwa wanaangua vilio.



Kutokana na gumzo hilo, Risasi Mchanganyiko lilimtafuta MC Pilipili na kumuuliza kuhusiana na kuangua kwake kilio ambapo alieleza kuwa alilia kutokana na changamoto alizokuwa amezipitia kwenye masuala ya uhusiano wa kimapenzi na msichana huyo.

Alisema hadi kufikia hatua hiyo ya kumvisha pete na binti huyo kukubali, halikuwa jambo rahisi bali alikumbana na ugumu hivyo alipoyakumbuka hayo, alijikuta machozi yakimtoka.



“Nimepata misukosuko mingi sana kwenye uhusiano ndiyo maana hadi machozi yamenitoka kwa furaha kwa kuwa nimefikia hatua nzuri, natarajia kuanza vikao vya maandalizi ya harusi hivi karibuni na vitakuwa vya muda mchache kwa kuwa ninataka kufanya haraka iwezekanavyo,” alisema MC Pilipili.



Kwa upande mwingine MC Pilipili alisema kuwa, ndoa yake itakayofanyika hivi karibuni inatarajiwa kuhudhuriwa na wageni waalikwa 2,000 ambapo wachekeshaji watakuwa ndiyo washehereshaji huku ikihudhuriwa na viongozi mbalimbali hivyo itakuwa ni harusi ya aina yake
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad