Steve Nyerere Apitia Kipindi Kigumu Sakata la Ommy Dimpoz

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Msanii wa Bongo movie Steve Nyerere amejikuta katika kipindi kigumu Baada ya kusema kuwa Ommy Dimpoz hataweza kurejea na kuimba vizuri kama zamani kwa kuwa hali yake kiafya si nzuri,

Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amejikuta akikaliwa kooni baada ya mashabiki wa Dimpoz kumjia juu na kumtaka atengue kauli yake kwani haikuwa nzuri hasa kwa Ommy Dimpoz ambaye anaumwa.

Gazeti la Ijumaa, Ommy Dimpoz alisema kuwa alichokizungumza ni kwamba, Dimpoz atachukua muda kurejea katika gemu tofauti na jinsi watu walivyomtafsiri kwamba hataweza kuimba kamwe.

Narudia kauli yangu nilisema hivi, atachukua muda kurudi katika gemu, kwa sababu hakuna mtu ambaye hajamuonea huruma Dimpoz wakati anaumwa, wote tulihuzunika, kwanza ni kijana mdogo amepita katika misukosuko mikubwa sana ya kimaradhi kwa hiyo sisi wote kama vijana tulimuonea huruma, ilitupasa sisi kama wasanii wenzake tuungane naye katika kipindi kile alichokuwa anapitia, lakini tunaamini kabisa kwamba itamchukua muda kurudi kwenye gemu na ndiyo kauli niliyosema mimi.
“Ni sawasawa na kocha akuambie kwamba itakuchukua muda kurudi kucheza mpira, kwa hiyo hayo maneno yanayosambaa huko mitandaoni sijui Steve kafanya hivi, sijui kafanya vile hayaniumizi kichwa hata kidogo, sina mamlaka ya kusema kwamba hataimba milele, mimi ni nani?”.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad