Serikari ya DRC Congo Yakiri Maafisa Kuhusika na Mauaji Katika Vijiji vya Yumbi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Serikari ya DRC Congo Yakiri Maafisa  Kuhusika na  Mauaji Katika Vijiji vyaYumbi
Serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo imekiri kwa mara ya kwanza kwamba maafisa wa serikali walitumika katika mauaji ya mamia ya watu mwezi Disemba mwaka jana.

Takriban raia 535 waliuawa kati ya tarehe 16 na 17 mwezi Disemba katika vijiji vitatu vya Yumbi , eneo la mashambani magharibi mwa DR Congo ukingoni mwa mto Congo yapata kilomita 350 kaskazini mwa Kinshasa.

Mauaji ya kikabila yalifanyika kwa siri kubwa mara ya kwanza kwa sababu yaliendeshwa siku kadhaa kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa urais.

Siku kadhaa zilipita na habari zikaanza kuchipuka na ilichukua takriban mwezi mmoja kabla ya kiwango cha muaji hayo kubainika.

"kile kilichotokea katika eneo la Yumbi mnamo mwezi Disemba sio kitu cha fahari kwa taifa langu'', alisema waziri wa mashirika ya haki za kibinadaamu nchini DRC Marie-Ange Mushobekwa ambaye kwa sasa yuko mjini Geneva.

"Wanasiasa na maafisa wa utawala walihusika katika mauaji hayo , na kusababisha ndoto mbaya tunayozungumzia kwa sasa," alisema Mushobekwa akidai kwamba mauaji hayo yanahusishwa na mzozo wa ardhi.

Mauaji hayo yalihusisha kukatwa mapanga kwa wanawake wajawazito pamoja na kunyofolewa sehemu zao za siri, alisema.

Waziri huyo alikuwa akizungumza katika mkutano wa baraza la Umoja wa mataifa kufuatia kuchapishwa kwa ripoti ya Uchunguzi wa Umoja wa mataifa mnamo tarehe 17 hadi 26 mwezi Januari.

Matamshi ya waziri huyo yanajiri huku wanaharakati wa haki za kibinaamu nchini humo wakishinikiza kuwasilishwa mahakamani kwa watuhumiwa wa mauaji hayo haraka iwezekanavyo.

Mwanaharakati wa haki za kibinaadamu Jean Claude Katende anasema kuwa mashirika hayo yanataka kujua ni akina nani waliohusika kupanga mauaji hayo upande wa serikali pamoja na upande wa raia.

Wakimbizi 18 wa Burundi wauawa DR Congo
''Tunataka kujua kwa nini walifanya hivyo hatujui walitaka kuzuia uchaguzi ama sijui kwa malengo yapi. Kwa sasa tunasubiri ripoti ya makundi ya haki za kibinadamu juu ya mauaji hayo'', alisema bwana Katende
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad