Wanaosambaza Uzushi Kuhusu Samatta Waonywa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Wanaosambaza uzushi kuhusu Samatta waonywa
Shirikisho la soka nchini (TFF), limekanusha taarifa zinazosambaa mtandaoni, kuhusu nahodha wa timu ya taifa Mbwana Samatta, kuwa amesema Taifa Stars haina nafasi ya kufuzu AFCON 2019.

TFF kupitia taarifa yake imeeleza kuwa taarifa hizo si za kweli na ni za uzushi huku ikisisitiza kuwa nyota huyo hajafanya mazungumzo na chombo chochote cha habari.

''Samatta hajaongelea mchezo wa Jumapili popote pale, zaidi tu anasisitiza mshkamano, kabla, wakati na baada ya mchezo'', imeeleza taarifa hiyo.

Aidha taarifa imeeleza kuwa Samatta amewaomba mashabiki wajitokeze kwa wingi uwanjani siku ya mchezo kwaajili ya kuipa nguvu timu dhidi ya Uganda ambao ni wa mwisho Kundi D.

Taifa Stars itakuwa inasaka nafasi ya kushiriki fainali za AFCON kwa mara ya pili baada ya mwaka 1980, endapo itaifunga Uganda na kufikisha pointi 8 kwenye kundi hilo linaloongozwa na Uganda wenye pointi 13.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad