AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Elizabeth Warren, aliyetangaza nia ya kuwania urais kupitia chama hicho, ameandika kwenye mtandao wa Twitter kwamba ripoti ya Mueller imeonesha ukweli kwamba "serikali hasimu ya kigeni iliushambulia uchaguzi wa 2016 kumsaidia Trump na mwenyewe Trump aliupokea msaada huo, na baada ya kuchaguliwa akataka kuzuwia uchunguzi dhidi ya mashambulizi hayo.
" Warren amesema sasa ni jukumu la Baraza la Congress kuchukuwa hatua za kukataa matumizi mabaya ya madaraka ili kulinda heshima ya utawala wa sheria.
Hata hivyo, spika wa Baraza la Wawakilishi kutokea chama cha Democrat, Nancy Pelosy, amesema hatopigania kura ya kumuondoa madarakani, ikiwa hakupata hakikisho la uungwaji mkono wa wajumbe wa Republican.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK