AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Musukuma ametoa kauli hiyo katika vikao vya Bunge kwenye mjadala wa Wizara ya Katiba na Sheria ambapo kupitia Waziri wa Katiba na Sheria, Agustino Mahiga aliwasilisha makadirio ya bajeti yake.
"Niseme tu kiukweli ni vizuri mkaangalia mkarekebisha sheria, hasa kwenye makosa madogodogo ambayo yamepelekea magereza mengi kujaa mahabusu ambayo kwa kweli mengine yanastahili makofi tu mtu akaenda nyumbani", amesema.
Musukuma ameongeza kuwa, "nashauri sana hizi sheria zilizotungwa tukiwa milioni 20, leo tuko milioni 55 mtu anawekwa wiki 2 kwa kesi ya kuiba kuku, ni vitu ambavyo tufikirie adhabu ili kupunguza mrundikano wa mahabusu kule ndani."
"Nilisoma kwenye kitabu cha Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuhusiana na uteuzi wa Majaji, inampa mamlaka Rais kuteua na anakuwa jopo la kumshauri ninawataka tu wenzangu wamuachie Rais akafanya majukumu yake." amemalizia Musukuma.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK