Ndugai: Bunge Halitafanya Kazi na CAG Professa Mussa Assad na Si Ofisi yake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Spika Ndugai: Bunge Halitafanya Kazi na CAG Professa Mussa Assad na Si Ofisi yake
Spika wa Bunge Job Ndugai amesema kwamba, Bunge limekataa kufanya kazi na mtu ambaye ni Profesa Mussa Assad, na siyo ofisi ya CAG, kama baadhi ya vyombo vya habari vilivyonukuu.

Ndugai ametoa kauli hiyo leo mchana Alhamisi Aprili 4, 2019 baada ya kuwatambulisha wageni walioalikwa bungeni.

"Bunge hili limekataa kufanya kazi na mtu anayeitwa Prof. Mussa Juma Assad, halijakataa kufanya kazi na Ofisi ya CAG, sisi kama Bunge hatujawahi kukataa kufanya kazi na taasisi yoyote" Amesema Spika Job Ndugai

Juzi, Aprili 2, 2019 Bunge lilipitisha azimio la kutofanya kazi na Profesa Assad kwa sababu ya kauli yake aliyoitoa wakati akihojiwa na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa kuwa Bunge ni dhaifu.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad