Rais Magufuli: Bila Mkapa Nisingekuwa Waziri, na Urais Yawezekana Msingeniona

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli amesema hatajali maneno ya watu ambao watasema kuwa yeye anajenga miundombinu kwenye Mkoa anaotoka Rais wa awamu ya tatu Benjamini Mkapa, kwa kuwa anajua alipomtoa.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo akiwa mkoani Mtwara kwenye uznduzi wa Kituo cha Afya Mbonde kilichopo Masasi ambapo

“Watu watasema ninamjengea Mkapa, ndio ni kweli ninamjengea Mkapa kwasababu bila yeye nisingekuwa waziri na inawezekana hata urais nisingepata kwahiyo kumjengea kabarabara tu nishindwe

“Ninafahamu Mkapa alinitoa wapi, yako maeneo ya barabara hii kilomita 40 mimi nimeyajua kuliko watu wa Mkoa huu kwasababu Mkapa alikuwa ananituma kwenda kufanya kazi.

"Tulipomaliza ujenzi wa daraja la Mkapa tulimwambia tunalipa jina lake akakataa lakini siku anaenda kulizindua alikuta tumeandika jina lake sasa hivi ana miaka karibu 80 haiwezekani kila anapokwenda mahali walipozikwa wazazi wake tushindwe kutengeneza barabara"

Kuhusiana na Waziri wa awamu ya tatu kupewa kiwanda cha korosho lakini hakiendelezi Rais Magufuli amesema; "kuna kiwanda naambiwa ni cha Waziri wa awamu ya tatu mumnyang'anye, akikataa shikeni pelekeni mahakamani hata kama alikuwa Waziri, tukibembelezana hatutafika ndugu zangu, tubembelezane mimi nikishamaliza muda wangu."

"Nitoe wito kwa waliouziwa viwanda vya kubangua Korosho na Serikali, ni lazima waanze kubangua Korosho na wazinunue, wakishindwa wavirudidhe viwanda, mfano yule wa Newala kiwanda hakifanyi kazi kabisa Waziri wa Kilimo mnyanganye hata kama ni leo." amemalizia Rais Magufuli

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad