Alichokifanya Masele baada ya Kuhojiwa...."Sijawahi kukurupuka, nasimamia haki na najitambua"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge imemhoji mbunge wa Shinyanga Mjini (CCM), Stephen Masele kuhusu tuhuma zinazomkabili za utovu wa nidhamu.

Masele alihojiwa na kamati hiyo inayoongozwa na  Emmanuel Mwakasaka  jana Jumatatu Mei 20, 2019.

Mara baada ya kutoka katika mahojiano Masele alizungumza na wanahabari, “Mimi ninaheshimu  sana viongozi wangu, nimelelewa vizuri na wazazi, nimelelewa vizuri na chama changu, nimetokea umoja wa vijana kuanzia ngazi ya chini kabisa mpaka ngazi ya kitaifa na kuwa mjumbe wa baraza kuu Taifa, nimekuwa mbunge hii awamu ya pili.

“Nimekuwa naibu waziri  natambua miiko ya uongozi, sijawahi kukurupuka, fuatilia rekodi zangu chochote ninachokisema ninasimamia haki, ukweli na ninaheshimu viongozi wenzangu.

“Ni matarajio yangu haki itatendeka na mimi sijafanya jambo lolote kinyume na taratibu, kwenye kazi zangu ndani ya Bunge na pia Bunge la Afrika kama makamu wa rais.”

Kuhusu utovu wa nidhamu amesema, “Nawahakikishia Watanzania, nilichokuwa nasimamia ni misingi ya haki za binadamu na kufanya hivyo nisitafsiriwe kwamba ni utovu wa nidhamu.”
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad