AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mganga mfawidhi wa hospitali hiyo Dk. Joakim Eyembe akizungumza na wauguzi baada ya kusikiliza kero zinazowakabili kuhusiana na vitisho toka kwa ndugu wa wagonjwa na wizi wa vifaa tiba na dawa, amewaondoa hofu kwa kuwaambia tayari kamera zimefungwa kila sehemu.
Dk. Eyembe akizungumza kupitia kilele cha maadhimisho ya siku ya wauguzi duniani katika viwanja vya hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mara, ameongeza kuwa wameamua kuajiri kampuni maalumu ya ulinzi ili kuweza kukabiliana na tatizo la wizi wa vifaa tiba unaodaiwa kufanywa na baadhi ya watu wanaoingia kwa kupitia katika uzio.
Wauguzi katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mara iliyopo mjini Musoma wamekuwa wakitoa huduma za afya kwa wagonjwa wengi kwa wakati mmoja kutokana na kuwa wachache wao baada ya zoezi la serikali kukabiliana na tatizo la vyeti feki.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK