‘Dada’ Afungwa Jela Maisha Kwa Kumuambukiza Mtoto wa Bosi Ugonjwa wa zinaa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mahakama ya Hakimu Mkazi Migori nchini Kenya, leo imemhukumu kifungo cha maisha jela mwanamke mwenye umri wa miaka 22, mfanyakazi wa ndani kwa kumbaka na kumpa ugonjwa wa zinaa mtoto wa kiume wa bosi wake.

Akisoma humu hiyo, Hakimu Mwandamizi, Raymond Langat ameeleza kuwa kulikuwa na vielelezo vya kutosha kuwa Machi 30, 2019 mwanamke huyo alitenda kosa hilo na kumuambukiza kwa makusudi mtoto huyo wa kiume.

Hakimu ameeleza kuwa Mahakama imefikia uamuzi wa kutoa adhabu hiyo baada ya kujiridhisha kuwa mshtakiwa alikuwa anatumia dawa za kutibu ugonjwa wa zinaa, hivyo alikuwa na nia ya kumuambukiza mtoto huyo.

Imeelezwa mahakamani hapo kuwa mtoto huyo ambaye hivi sasa anapatiwa matibabu maalum, alipata madhara makubwa ya kisaikolojia kutokana na tukio hilo.

Kwa mujibu wa Citizen TV, Mshtakiwa huyo amepewa siku 14 za kukata rufaa kama hajaridhishwa na uamuzi huo wa mahakama, vinginevyo atatakiwa kutumikia kifungo cha maisha jela.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad