AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Jumatano Juni 19, Kamanda wa Kanda Maalumu Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, amesema mtuhumiwa huyo amekamatwa usiku wa kuamkia leo maeneo ya Madale.
“Mtuhumiwa katika mahojiano na Jeshi la Polisi amekiri kumchoma kisu kilichosababisha kifo cha mwanafunzi huyo huku akieleza namna mwanafunzi huyo alivyokuwa amevaa siku hiyo ya tukio kuwa ni fulana nyeusi, suruali ya ‘jeans’ na kapelo nyeusi.
“Aidha mtuhumiwa alikiri kumpora pochi iliyokuwa na simu moja aina ya Tecno rangi nyeusi, fedha taslimu Shilingi 8,000 na vitambulisho mbalimbali ambavyo alivitupa na simu hiyo kuiuza,” amesema Kamanda Mambosasa.
Mtuhumiwa anaendelea kushikiliwa kwa mahojiano zaidi na atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK