AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza na Spoti Xtra Waziri Mwakyembe amewataka Watanzania kwa jumla kuungana katika hafla hiyo ambayo chochote kitakachopatikana kitakwenda moja kwa moja kwenye mifuko ya wachezaji. Hafla hiyo itaanza saa 4 asubuhi mpaka jioni.
“Hiki tunachokifanya ni sehemu ya uzalendo kuonyesha kuwa tupo pamoja na wanajeshi wetu watakaokuwa wanapambania heshima ya nchi yetu kule Misri.
“Pesa tunayochangisha inakwenda moja kwa moja kwenye mifuko ya wachezaji kwa sababu mambo mengine yote yameshafanyika, kama sehemu ya kulala, chakula na posho ndogo ndogo hivyo vyote serikali imeshafanya, lakini hii inakwenda kuwahamasisha ili wajue kuwa hawapo peke yao katika mapambano hayo,” alisema Mwakyembe.
Naye Mkurugenzi wa Maendeleo Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Yusuph Singo aliliambia Xtra kuwa; “Maandalizi yote yapo vizuri na muitikio ni mkubwa sana.”
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK