CCM yatoa onyo kwa viongozi hawa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Chama cha mapinduzi CCM kimetoa onyo kwa baadhi ya viongozi watakaotumika kuingiza mamuruki ya watu, ili kugombea nafasi katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajia kufanyika mwishoni mwa mwaka huu nchini kote.

Akiwa katika ziara ya siku moja mkoani Iringa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi Taifa Humfrey Polepole, amekemea vikali vitendo ambavyo vinatajwa kuwa mwiba kwa chama hicho na kusababisha kushindwa katika chaguzi jambo ambalo amesema halivumiliki.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Iringa Dtk Abel Nyamahanga amewataka wanachama na viongozi wa chama hicho, kushikamana ili kuibuka na ushindi katika chaguzi zijazo ikiwemo uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka 2020.

Ziara ya Polepole imelenga kuwajengea uwezo viongozi wa mitaa wakiwemo wenyeviti wa mitaa, Mabalozi na makatibu kata wa chama hicho katika Manispaa ya Iringa, ili kujiandaa na uchaguzi wa serikali za mitaa.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad