Iran yawakamata majasusi 17 wa CIA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Iran inasaema imewakamata majasusi 17 wanaofanya kazi katika Shirika la Ujasusi la Marekani, CIA, na wengine wamehukumiwa adhabu ya kifo.

Televisheni ya taifa ya Iran imemnukuu afisa wa wizara ya ujasusi akisema kuwa pia imelivunja genge la majasusi hao.

Afisa huyo amesema waliokamatwa wamehukumiwa adhabu ya kifo.

Tangazo hilo limetolewa miezi mitatu tangu kuzuka kwa mvutano na mataifa ya Magharibi ulioanza wakati Marekani ilipoweka vikwazo vikali kwa Iran ambavyo vilianza rasmi mwezi Mei.

Wiki iliyopita, Iran iliikamata meli ya mafuta yenye bendera ya Uingereza katika Mlango Bahari wa Hormuz, baada ya Uingereza kuikamata meli ya mafuta ya Iran kwenye pwani ya Gibraltar, Julai 4.

Haijajulikana wazi kama kukamatwa majasusi hao kunahusiana na kesi ambayo Iran ilisema mwezi Juni kuwa imegundua mtandao mkubwa wa kijasusi iliyodai unaendeshwa na CIA na kwamba majasusi kadhaa wa Marekani walikamatwa katika nchi tofauti.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad