Ukaribu Wenye Maswali wa Polisi na Vyama vya Kisiasa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Katiba ya Jamhuri ya Muungano ibara ya 147(3) inasema, “Itakuwa ni marufuku kwa mwanajeshi yeyote kujiunga na chama chochote cha siasa, isipokuwa tu kama atakuwa na haki ya kupiga kura iliyotajwa katika ibara ya 5 ya Katiba hii.”

Na kifungu cha nne cha ibara hiyo, kinaeleza maana ya “mwanajeshi” kuwa ni askari aliyeajiriwa kwa masharti ya muda au ya kudumu katika Jeshi la Ulinzi, Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza au Jeshi la Kujenga Taifa.

Pamoja na suala hilo kuzuiwa katika Katiba, siku za hivi karibuni kumekuwapo na matukio yanayoambana na kauli za viongozi yakiashiria matumizi ya baadhi ya wanajeshi kushiriki au kushirikishwa katika shughuli za kisiasa, huku CCM ikionekana kunufaika na utaratibu huo.

Hali hiyo inayozua mjadala inajidhihirisha kupitia kauli za baadhi ya viongozi wa Jeshi la Polisi, mfano ile ya kamanda wake wa Mkoa wa Arusha, Jonathan Shanna akiwa katika mkutano wa ndani wa CCM.

Akizungumza katika mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa AICC, Kamanda Shanna akieleza kuwa vyombo vya dola ni sawa na CCM.

“Kuna hesabu darasa la nne inasema kama A ni sawa na B na B ni sawa C, kwa hiyo A ni sawa na C. Maana yake A ni chama tawala na B ni Serikali halali na C ni vyombo vya dola ndiyo sisi. Sasa kama chama tawala, Serikali, vyombo vya dola, sasa wewe jiulize A kama is equal to C maana yake nini?”

 By Elias Msuya, Mwananchi emsuya@mwananchi.co.tz
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad