Bilionea Yanga Amjibu MO kitemi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


MASHABIKI wa soka wamekuwa wakichonga sana dhidi ya Yanga kutokana na bilionea wao, Mohammed ‘MO’ Dewji kumwaga mzigo wa maana Msimbazi na kelele zilizidi baada ya kuzindua jezi mpya zenye chata ya Mo Halisi juu mgongoni.

Mashabiki hao wamedai namna jezi za Simba zinavyoanza kuchafuka ni dalili njema ya kufuata mkumbo wa klabu kubwa Afrika na Duniani kuwa na machata yanayowaingizia fedha na hivyo ishu za kutembeza bakuli kama watani zao haitakuwapo.

Lakini sasa unaambiwa kilichofanywa na bilionea aliyeamua kumwaga fedha Jangwani kupitia udhamini wa jezi, ni kama vile amemjibu MO Dewji kibabe baada ya kutangaza mkwanja mwingine wa maana kupitia bidhaa zinazozalishwa na kampuni yake ya GSM.

Si mnajua kampuni hii inamilikiwa kigogo mmoja mwenye fedha zake za maana, Ghalib Said Mohammed, ambapo kampuni yake ndiyo inayosambaza jezi za Yanga msimu huu baada ya kuingia nao mkataba mnono ambao hata hivyo thamani yake haitajwi.

Sasa wakati hata mkataba wa mwanzo haujakauka wino, bilionea huo ameamua kumwaga mamilioni Jangwani kwa kuingia mkiataba wa mwaka mmoja wa kuidhamini Yanga kupitia magodoro yanayozalishwa na kampuni hiyo ya GSM ambayo chata lake litakaa mgongoni.

Tayari Yanga na GSM Foam, wamesaini mkataba huo na kwa sasa sasa jezi za Yanga nazo zitakuwa kama zile za watani wao, ukiacha jina la mchezaji mgongoni pia litakuwa na chata la GSM Foam na kuzidi kuineemesha klabu hiyo kifedha.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad