AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha, Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo, Steven Mlote amesema kuwa taarifa hizo hazina ukweli wowote, hakuna mfanyakazi aliyeacha kazi na wale ambao hawapo wako likizo.
Amesema kuwa Jumuiya hiyo haina tatizo la ukata wa fedha kama taarifa zinavyoenezwa, kwani shughuli za jumuiya hiyo zinaendelea kama kawaida na wafanyakazi wanaendelea na majukumu yao kama kawaida.
”Taarifa zilizosemwa kwamba wafanyakazi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wamekimbia ofisi sio za kweli, ukweli ni kwamba wako kazini, wanafanyakazi kwa weledi na Jumuiya iko salama na inaendelea kuimarika,”amesema Mlote
Aidha, kwa muda wa wiki moja sasa kumekuwepo na taarifa zinazosambaa kwamba wafanyakazi wa jumuiya hiyo wameikimbia ofisi kutokana na ukata wa fedha, ambao umesababisha wafanyakazi hao kutolipwa mishahara.
Hata hivyo, Mlote ameongeza kuwa changamoto zilizopo katika ofisi hiyo ni za kawaida, hivyo nchi wanachama wa jumuya hiyo zinaendelea kuchangia michango yake kama kawaida.
Jumuiya hiyo inaundwa na nchi wanachama, ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Sudan Kusini, Rwanda na Burundi.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK