Mbaroni Kwa Kosa la Kumbaka Mtoto wa Miaka Mitatu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

JESHI la polisi mkoani Pwani, linamshikilia Dismas Silyvester (35)  kwa kosa la kumbaka mtoto mdogo mwenye miaka mitatu, huko Mlandizi  A ,kata ya Mlandizi ,Kibaha .

Aidha Mariam Shomari (25) mkazi wa Msongola ,Mlandizi Kibaha ameibiwa mtoto wake mchanga wa miezi mitatu katika mazingira ya kutatanisha ambapo jeshi hilo linaendelea na msako ili kumpata mtoto huyo.

Akithibitisha kutokea kwa tukio la kwanza ,kamanda wa polisi mkoani hapa, Wankyo Nyigesa aliwaambia waandishi wa habari kwamba, Dismas alimuiba mtoto wa miaka mitatu na kwenda nae kichakani na kumfanyia unyama huo.

“Baada ya taarifa kutolewa kwa jeshi la polisi kwa kushirikiana na raia wema lilimkamata mtuhumiwa na mtoto mchanga huyo katika mashamba ya mbogamboga vichakani “alifafanua Wankyo.

Wankyo alieleza ,uchunguzi unaonyesha mtoto huyo ambae jina limehifadhiwa ,ameingiliwa kimwili.

Akielezea tukio jingine Wankyo alisema, agost 25 saa 7 mchana ,Msongola, Mariam Shomari aligundua kuibiwa mtoto wake mchanga Swaumu Sudi mwenye miezi mitatu.

“Mtoto huyo aliibiwa ndani akiwa chumbani alipokuwa amelala baada ya mama yake kutoka kwenda kuomba kibiriti kwa jirani umbali wa mita 200 na mwanamke ambae hajafahamika hadi sasa”

Inadaiwa mwizi huyo wa mtoto alitumia mbinu ya kuvizia mama wa mtoto kutoka na yeye kufika kwenye nyumba hiyo na kumwambia mtoto mdogo Fatima Sudi miaka mitatu aliyekuwa amebaki na mdogo wake kuwa ametumwa na mama yake kuja kumchukua mtoto huyo ili ampelekee na kufanikisha wizi huo.

Jeshi hilo linaendesha msako mkali wa kumtafuta mwizi wa mtoto ambapo ametoa wito kwa viongozi wa serikali za mitaa ,watendaji wa kata ,wenyeviti wa vitongoji na vijiji pamoja na jamii kutoa taarifa iwao watamtilia shaka mtu ambae anaonekana na mtoto asiye wake.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad