VIDEO: Alalamika Kurushiwa Mawe Yenye Moto juu ya bati, Mrushaji Haonekani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mkazi wa kijiji cha Tindigani wilayani Siha mkoani Kilimanjaro anyejulikana kwa jina la Godfrey Nasary amesema amekuwa akirushiwa mawe kwa zaidi ya siku 20 bila kumuona anayerusha mawe hayo huku yakiharibu nyumba yake ikiwemo mabati pamoja na vioo.

Amesema wakati akiwa na wachungaji wanaomba wanashangaa mawe yanarushwa na kuna siku jiwe lilirushwa likiwa linawaka moto huku akihusisha suala hilo na mambo ya kishirikina.

“Sasa hivi ni wiki mbili na zaidi kwamba yaliibuka tu mawe yakirushwa juu ya bati, mawe ni makubwa ambayo yanarushwa nyakati za usiku. Siku nyingine yanaanza mchana kuanzia saa 11 mpaka kwenye muda wa saa tatu. Wachungaji wamekuwa wakifanya maombi na sisi pia huwa tunafanya maombi. Ukifika wakati wa maombi ndiyo kwanza wanachachamaa kurusha mawe.”

Amesema wamejaribu kufanya uchunguzi lakini mpaka sasa hawajagundua anayefanya tukio hilo, hivyo kuingiwa na hofu kubwa.

Amesema mawe hayo yameharibu sana mabati ya nyumba yake kiasi kwamba yamekuwa hayafai tena na ikiwa mvua itanyesha basi nyumba itakuwa ikivuja.

Amesema maeneo mengine ya nyumba ambayo yameathiriwa na mawe hayo ni madirisha na sehemu za milango ambazo zimenakshiwa na vioo.

Zaidi angalia video hii;
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad