AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Katika kesi hiyo namba namba 98 ya mwaka 2019, iliyosomwa leo Septemba 20, 2019, na Wakili wa Serikali Mkuu, Faraja Nchimbi, mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Kelvin Mhina, Mgoli amesomewa mashtka matatu.
Shtaka la kwanza anatuhumiwa kwa kujifanya ofisa wa TISS, kosa ambalo alilitenda kati ya Desemba 1, 2017 na Agosti 2019, katika eneo la Mahabusu ya Keko.
Katika shtaka la pili, Mgoli anatuhumiwa kujiingizia pesa kwa njia ya udanganyifu ambapo Agosti 17, 2019 na 29 Agosti 2019 alijipatia kiasi cha Tsh. 280,500 kutoka kwa Lucy Ngongoseki akiwa eneo la Mahabusu ya Keko akijifanya Ofisa Usalama ambaye alidai atamsaidia kwenye kesi namba 213 ya mwaka 2017 inayomkabili Jamali Malinzi ya uhujumu uchumi inayomkabili Jamal Malinzi.
Katika Shtaka la tatu mtuhumiwa anadaiwa kufanya utakatishaji fedha haramu katika tarehe 17 Agosti 2019 na 29 Agosti 2019 akitumia pesa kiasi Tsh 280,500 ilhali alijiua ni zao la kosa tangulizi la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
Baada ya kusomewa mashitaka hayo, Hakimu Mhina alisema mahakama hiyo haina mamlaka ya kumpatia mshitakiwa dhamana, pia haina mamlaka ya kusikiliza kesi ya uhujumu uchumi, hivyo mshtakiwa atakwenda rumande. Upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika, ambapo kesi imeahirishwa hadi Oktoba 4, 2019.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK