AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Waziri Mkuu wa Zamani wa Tanzania, Edward Lowassa amepongeza utendaji kazi wa Rais John Pombe Magufuli ambapo amesema kampeni yakutumbua watu ambao ni wazembe imesaidia nchi kushika adabu na mambo yanakwenda kwa utaratibu
Lowassa ameyasema hayo jana katika mahafali ya shule ya msingi ya Meyers mjini Arusha.
"Rais Magufuli anastahili pongezi anafanya kazi nzuri sana, tunaona mawaziri wanafanya kazi nzuri , Waziri Mkuu (Kassim Majaliwa) yupo kule wengine huku, nchi imewaka moto kila sehemu.” Amesema Lowassa
Kwa mujibu wa Lowassa, kazi za Rais Magufuli, zinatakiwa kupakwa ‘poda’ kwa kuhusisha uboreshaji wa elimu ambayo itawapa ujuzi wahitimu kujiajiri.
"Kuna vijana wengi wanamaliza masomo kutokana na mpango wa elimu bure sasa tujitahidi elimu hii iwasaidie vijana kupata ujuzi na ubunifu ili kuweza kujiajiri."Ameongeza Lowassa.
Lowassa aliyejiunga ndani ya Chadema tarehe 28 Julai 2015 na kupitishwa kuwa mgombea urais wa chama hicho akiungwa mkono na vyama rafiki vya Ukawa, alishindwa kuhimili mikikimikiki ya upinzani na kuamua kurejea ndani ya chama tawala CCM tarehe mosi Machi mwaka huu.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK