Mugabe Kuagwa Jumamosi, Mazishi Yaandaliwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwili wa Rais wa zamani wa Zimbabwe, Robert Mugabe unaotarajiwa kuzikwa jumapili hii septemba 14, nchini humo unatarajiwa kuagwa siku ya jumamosi.

Mwili huo unatarajiwa kurejeshwa nchini Zimbabwe kesho kutoka Singapore alipokuwa akipatiwa matibabu hadi umauti ulipompata.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na mpwa wa marehemu Mugabe, familia yao bado haijafahamu Rais huyo wa kwanza wa Zimbabwe atapumzishwa wapi, japo wanaamini mazishi yatafanyika katika makaburi ya Mashujaa ya Taifa, kama ilivyokuwa imepangwa kabla ya kuondolewa madarakani mwaka 2017.

Katika makaburi hayo ya mashujaa yaliyojengwa kwa msaada wa Serikali ya Korea kaskazini, ndipo alipozikwa mke wake wa kwanza, Sally Mugabe ambaye alikuwa ni moja ya wanaharakati wa ukombozi wa Zimbabwe, aliyetazamwa na wengi hadi kifo chake kama ni mama wa Taifa la Zimbabwe.

Aidha taarifa zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari nchini humo, zinaeleza kuwa baadhi ya ndugu zake wanataka azikwe kijijini kutama, alipozaliwa katika jimbo la Magharibi mwa mji mkuu, Harare.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad