Prezzo Ajitupa rasmi kwenye siasa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Msanii wa muziki wa Hip Hop nchini Kenya, Jackson Makini almaarufu kwa jina la Prezzo ametangaza rasmi kuingia kwenye siasa kwa kuchaguliwa nafasi ya kugombea ubunge katika jimbo la Kibra nchini humo.



Prezzo ameteuliwa na Chama cha Wiper leo Jumanne Septemba 10, 2019,  mbele ya kiongozi wa Chama hicho,  Kalonzo Musyoka ambaye alishawahi kuwa makamu wa Rais wa Taifa hilo.

Taarifa hiyo imepokewa na kwa mikono miwili na Wakenya, Huku wengi wakimlinganisha na msanii mwenzie wa muziki, Jaguar ambaye yeye kwasasa ni Mbunge wa Jimbo la Starehe.

Kalonzo anaamini kuwa kutokana na ukumbwa wa Prezzo,  Anauwezo mkubwa wa kuchukua jimbo hilo kwenye uchaguzi utakaofanyika Novemba 7 mwaka huu.

Prezzo atapambana na mwakilishi mwingine wa Chama cha ODM, Imran Okoth kwenye kinyang’anyiro cha kusaka ubunge kwenye jimbo hilo la Kibra.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad