AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Amesema kuwa vyombo vya habari hivyo hususani ‘Online TV’ zaidi ya 15 zilichapisha na kutumia picha mbalimbali za miili ya watu waliofariki katika ajali kinyume na kanuni, miiko na maadili ya uandishi
Baadhi ya Viongozi wa vyombo vya habari walikiri makosa hayo na kuomba radhi mbele ye Kamati ya Maadili ya TCRA walipoitwa kuhojiwa.
Viongozi wa Lemutuz Online TV na Global TV, vituo vilivyochapisha picha hizo, walifika mbele ya Kamati Agosti 28 kwa kushindwa kujirekebisha ndani ya muda wa Kanuni
Le Mutuz ilieleza kuwa kosa hilo lilisababishwa na uzembe wa Msimamizi wao wa maudhui ambaye hakutumia busara na weledi katika uchapishaji wa video ile.
Aidha, Global TV ilisema kuwa ilichukua tahadhari kubwa ya kuziziba picha kwa kuweka kivuli lakini kulitokea tatizo la kiufundi na picha hizo zikaonekana.
Hata hivyo, baada ya utetezi wa viongozi hao wa Kamati ya maudhui ilivipa onyo kali chaneli hizo na kuziamuru kuomba radhi kupitia chaneli hizo kwa siku 7 mfululizo kuanzia Septemba 07.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK