RC Makonda akoshwa na upepo wa kisulisuli ‘Heri kelele za watu wanaomuomba Mungu kuliko za Bar’

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Mhe. Paul Makonda amewaomba viongozi wa Dini mbalimbali kwa imani zao, Watangaze Injili popote pale ndani ya mkoa huo bila wasiwasi wowote ule na serikali itawapa ushirikiano.



RC Makonda akiongea leo Jumatatu Oktoba 28, 2019 katika kongamano maalum lililoandaliwa kuelekea Uchaguzi, Uchumi wa viwanda, Amani, Mahusiano, Uzalendo na Ustawi wa Taifa, Amesema kuwa kuna watu wanaona kuomba usiku ni kama kupiga makelele lakini ni bora wanaopiga kelele za kumuomba Mungu kuliko kelele za Baa.

Kwa upande mwingine, RC Makonda amesema kuwa alikuwa hajui ‘Upepo wa Kisulisuli’ umeandikwa kwenye Quran huku akidadavua kuwa upepo huo kuna watu wanauelezea kwa maana zao lakini kiimani kuna watu unawaponya.

Kauli hiyo ya RC Makonda inakuja ikiwa wiki moja iliyopita DC Ilala, Sophia Mjema akaririwe na vyombo vya habari akisema siku za kusali ni tatu tu kwa wiki yaani Ijumaa, Jumamosi na Jumapili.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad