Mkuu wa Mkoa Aamuru Mkandarasi Manispaa ya Bukoba na Mkuu wa Shule Wakamatwe na Kuwekwa Ndani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mkuu wa mkoa Kagera Brigedia Marco Elisha Gaguti amemuagiza Kamanda wa polisi mkoani humo Revocatus Malimi kuwakamata na kuwaweka ndani mara moja mkandarasi wa manispaa ya Bukoba, Mkandarasi wa  Kampuni ya Mzinga Holding Company ambaye pia ni msimamizi wa ukarabati wa Shule ya Sekondari Kahororo, mkuu wa shule ya Sekondari Kahororo pamoja na kaimu mkuu wa shule ya  Bukoba secondari kutokana na kushindwa kukamilika kwa ujenzi wa miundombinu ya shule hizo kwa wakati uliopangwa.

Hayo yamejili  Novemba 22,2019 baada ya Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa pamoja na kamati ya  Manispaa ya Bukoba Mkoani humo ilipofanya ziara mbalimbali ili kukagua baadhi ya miradi kwa upande wa manispaa ya Bukoba ikiwemo elimu, afya,pamoja na miundombinu ya barabara.

Waliokamatwa ni Mhandisi wa manispaa ya Bukoba bw,George Geofrey, Mkandarasi wa  Kampuni ya Mzinga Holding Company ambaye pia ni msimamizi wa ukarabati wa Shule ya Sekondari Kahororo,bw Festo Talimo ,Mkuu wa Shule ya sekondari kahororo bw Omary Ogambage pamoja na makamu mkuu wa Shule ya Sekondari Bukoba bw,Phocus Siasa.

Akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wasimamizi wa miradi hiyo mkuu wa mkoa wa kagera Brigedia Gaguti amesema kuwa miradi hiyo kwa ujumla mpaka hivi sasa haifanyi vizuri na kutoa msisitizo kwa watu wanaosimamia miradi hiyo kukamilisha kwa wakati na muda uliopangwa pasipo  kuomba muda wa nyongeza.

“ Watendaji waliopewa dhamana ya kusimamia miradi hiyo  wasimamie ili iweze kukamilika kwa muda uliopangwa lakini pale ambapo kuna uzembe tuliokuwa tukiuona  katika baadhi ya maeneo tutachukua hatua sitahiki ”

Ameongeza kuwa ataendelea kuchukua hatua stahiki kwa watendaji wa miradi hiyo watakaoshindwa kukamilisha kwa wakati  miradi hiyo na hakuna mkandarasi atakayeondoka mkoani Kagera kabla ya kukamilisha mradi anao simamia.

Kadhalika Brigedia Gaguti amesema kuwa miradi hiyo imepokea shilingi bilioni 12 kutoka fedha za serikali kuu kwa mwaka wa fedha kwa upande wa manispaa ya Bukoba mkoani humo na kuwataka wakandarasi kuongeza kasi ili wasije kulipa dhamana yao kwa uchungu huku akihaidi ushirikiano wa kutosha kwa wasimamizi wa miradi hiyo pale watakapo kuwa wamekwama.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad