Halima Mdee Achaguliwa Kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chadema (BAWACHA)

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mbunge wa Kawe, Halima Mdee amechaguliwa tena kuwa mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la Chadema (Bawacha) baada ya kupigiwa kura 317 za ndio.

Katika uchaguzi huo ulioanza jana Alhamisi Desemba 12,2019 na kumalizika leo Ijumaa Desemba 13, 2019 Mdee alikuwa mgombea pekee kwenye nafasi ya uwenyekiti .

Matokeo ya Uchaguzi huo yametangazwa leo Disemba 13, 2019, ambapo kupitia ukurasa wa Twitter wa chama hicho ukatoa mchanganuo wa Mwenyekiti pamoja na Makamu Mwenyekiti Tanzania Bara na Zanzibar.

"Mkutano Mkuu wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha) ulioanza jana asubuhi, umemalizika asubuhi hii ambapo umemchagua Halima Mdee kuwa Mwenyekiti wa Bawacha Taifa" imeeleza taarifa hiyo.

Aidha katika Uchaguzi huo Hawa Mwaifunga, amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bawacha Tanzania Bara, huku Sharifa Suleiman, akichaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti Zanzibar.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad