Lusinde 'Alipuka' Bungeni....Asema barabara kuelekea hospitali ya Mvumi imeoza

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mbunge wa Mtera (CCM), Livingstone Lusinde amesema hali ya barabara kuelekea hospitali ya Mvumi imeoza hivyo ni hatari kwa maisha ya watu.

Katika swali la nyongeza bungeni leo Jumanne Januari 28,2020, Lusinde amesema umuhimu wa hospitali ya Mvumi Mission unapotea na uzuri wa hospitali hiyo unakosekana kama hakutakuwa na barabara ya lami.

"Hata hiyo kilomita moja wanayosema imeanza kujengwa naona wamemdanganya Waziri, hakuna kitu, hali ni mbaya hasa kwa akina mama wanaohitaji huduma za hospitali hiyo na barabara nyingi nchi nzima zimeoza kabisa, nini mpango wa serikali katika eneo hilo," amehoji Lusinde.

Mvumi ndiyo hospitali kongwe kwa ajili ya wenye matatizo ya macho na kwa sasa ndiyo hospitali teule ya wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma.
 
Katika majibu ya serikali, Naibu Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tamisemi, Mwita Waitara amesema kutokana na umuhimu wa hospitali hiyo, wameanza maandalizi ya ujenzi wa kiwango cha lami barabara hiyo.

Waitara amesema kwa kuanza wamepanga kujenga barabara hiyo kwa urefu wa kilomita moja kazi itakayokamilika Agosti 2020.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad