Niyonzima Sasa Aanza Kuwaza Ubingwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



KIUNGO wa Yanga, Haruna Niyonzima raia wa Rwanda amefunguka kuwa, iwapo watashirikiana kwa pamoja wachezaji wote na benchi la ufundi ana uhakika wa timu yake hiyo kutwaa ubingwa wa ligi msimu huu.

 

Niyonzima amesajiliwa katika usajili wa dirisha dogo kwa lengo la kuongeza nguvu katika kikosi hicho kuhakikisha kinafanya vyema na kutwaa ubingwa wa ligi.

 

Yanga kwa sasa ipo nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi ikiwa na pointi 37, huku wakiwa  wamepishana pointi 16 na watani wao Simba wenye pointi 50.

 

Hii ni kabla ya mechi za jana. Akizungumza na Championi Jumatano, Niyonzima alisema kuwa, kama mchezaji dhamira yake ni kuonyesha kile alichonacho ndani yake kwa kuisaidia timu ili iweze kufanya vizuri kwenye ligi kwa kushirikiana na wenzie

“Nafasi ya ubingwa kwa Yanga bado ipo licha ya kutanguliwa katika msimamo wa ligi, tukishirikiana kwa pamoja bado tuna nafasi sana ya kuweza kufika kule tunapopahitaji, tuna kikosi kizuri na chenye ushindani.

“Kwa upande wangu najitahidi kuonyesha kile ambacho naona ni kizuri kwa manufaa ya timu kwa kushirikiana na wachezaji wenzangu,” alisema Niyonzima.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad