Hatimaye Chris Mauki Asimama na Kuwaomba Msamaha Wanaume "Naomba Mniwie Radhi "

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Baada ya Chris Mauki Kuwakwanza Wanaume wengi kwa post yake ya leo Instagram, Mwenyewe ameamua kuwaomba msamaha wanaume kwa kupitia post hii hapa chini:

chrismauki_
"Nichukue nafasi hii kwa unyenyekevu sana kueleza maana tarajiwa ya ujumbe wangu ambao umeonekana kuwakwaza wanaume wengi ambao ninauhakika tumetofautiana tu kwenye tafsiri na kama wewe ni mmoja wao unisamehe sana kwa hilo. Mimi pia ni mtafutaji wa chini tu, nimekuzwa kwenye familia ya baba mtafutaji wa kawaida tu kwa hali hii siwezi kamwe kudharau utafutaji wowote wa mwanaume wakitanzania. Nia yangu ilikuwa kuonyesha uhalisi wa baadhi yetu wenye tabia sugu ya kukwepa majukumu ya kuitunza familia kwa kujitetea kuwa sina au sijapata na wakati mke na watoto wanajua sio kweli kuwa baba hana. Baba anaweza kusema sina ila mke na watoto wanaona kunavitu anafanya vinavyoonyesha anahela. Ingawa pia wapo wanaokwepa majukumu yao kwa kudhamiria kabisa. Haya yapo na nyie mnajua ni kweli yapo. Kama kosa ni kutumia neno "msanii" hapo naomba mniwie radhi, sikuwa na nia ovu. Ninakubali kabisa kwamba maranyingine tafsiri ya mmoja inaweza isiwe tafsiri ya mwingine. Amani." Mauki
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad