Felix Mkosamali Ahama NCCR- Mageuzi na Kutimkia CHADEMA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Aliyewahi kuwa Mbunge wa Muhambwe Mkoani Kigoma kupitia Nccr-Mageuzi Felix Mkosamali, amekihama chama cha NCCR-Mageuzi na kujiunga na  Chadema nakutangaza nia ya kuwania ubunge wa Jimbo la Muhambwe kupitia CHADEMA katika uchaguzi mkuu mwezi Oktoba.

“Nimehama chama cha NCCR-Mageuzi kwasababu kimekuwa kama kinyonga hakieleweki kipo CCM au upinzani, ni chama ambacho kimekuwa hakifanyi kazi yoyote ya kisiasa kwa miaka mitano sasa kimeanza kuweka wagombea kwenye majimbo ya Chadema,” amesema na kuongeza.

“Nimeona Chadema ndio chama sahihi kugombea ubunge kwasababu kuna wanasiasa wenye msiamamo wa kisaiasa na wenye kudai katiba mpya”.

Amesema kuwa amekihama chama hicho ili aendelee kupigania mambo ya msingi na si kujipendekeza na kuwa anaamini wanaohama vyama ni haki yao lakini wengi wanaitumia vibaya haki hiyo kwasababu ya njaa na kushibisha matumbo yao.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad