Hatimaye Rais Kenyatta Afunguka Ukweli Mchungu..."Hali ya Kutoaminiana ni Tishio Kubwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Akijibu swali kutoka kwa mmoja wa washiriki wa mkutano huo, ambao kimsingi ulikuwa unajadili mahusiano a kibiashara kati ya Kenya na Marekani na mstakabali wa makubaliano yaliyotiwa Saini mapema mwaka huu kati yake na Rais Donald Trump, Kenyatta alisema mchakato wa kuimarisha jumuiya ya Afrika Mashariki umekabiliwa na changamoto chungu nzima.

“Tunakabiliwa pia na changamoto kubwa kutokana na sababu mbalimbali. Na pia kuna hali ya kutoaminina kati ya mambo mengine. Hii ndiyo imani niliyo nayo.. kwamba ni lazima tukabiliane na changamoto hizi, na njia ya kukabiliana nazo ni kuja pamoja na kushirikiana,” alisema.

Aidha alizungumzia juhudi za kuleta uwiano baina ya jamii zainazoishi kwenye mipaka ya nchi husika, akitaja Uganda na Ethiopia kama mfano, ambapo Kenya na serikali za nchi hizo zilifikia makubaliano ya jinsi ya kufanya biashara kwa raia wa pande zote kwenye mipaka ya nchi hizo.

Lakini licha ya taarifa za kidiplomasia zinazotolewa na viongozi mara kwa mara kuhusu utangamano wa kieneo, wachambuzi wamemekuwa wakitilia shaka kama baadhi wa viongozi wa kanda ya Afrika Mashariki wana imani ya dhati na ushirikiano huo, licha ya mikakati ambayo imeendelea kupigiwa upatu na baadhi yao, mchakato ambao umekuwa ukiendelea kwa miongo kadhaa tangu kuvunjika kwa jumuiya ya zamani ya Afrika Mashariki mnamo mwaka wa 1976.

“Makosa yaliyotokea mnamo miaka ya sabini na ya sitini yaliyopelekea kuvunjika kwa jumuiya ya zamani ya Afrika Mashariki, bado yapo, na hali ya kutoaminiana bado ipo kwa kiasi fulani. Mimi nimekuwa katika msitari wa mbele nikisema kwamba yaliyopita si ndwele na tunaweza kujifunza kutokana na makosa yetu ya zamani,” aliongeza Kenyatta.

Wakati wa mkutano huo wa Alhamisi, Rais Kenyatta pia alisisitiza kwamba hana nia ya kwendelea kuwa rais wa Kenya baada ya muhula wake wa pili kuisha, akisema kuwa Wakenya wanataka katiba, inayompatia kila rais mihula miwili ya mika mitano, iheshimiwe. Hata hivyo, alipoulizwa iwapo ana nia ya kuwa waziri mkuu baada ya kipindi chake cha urais kukamilika, kiongozi huyo alisema hana Habari kama kutakuwa na nafasi kama hiyo iwapo katiba itafanyiwa marekebisho.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad