Chifu Alia na Mtendaji Aliyekata Mti wa Kimila “Rudisha Mizimu Yangu”

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Chifu wa kabila la wagogo, Henel Mazengo wa pili, amemtupia lawama Ofisa Mtendaji wa kata ya Mvumi Makulu, Chamwino jijini Dodoma kwa kukata mti wa kimila.

Chifu Mazengo ameeleza kitendo cha kukatwa kwa mti huo kimemuondolea mizimu yake aliyokuwa anatumia kwenye kazi zake za kimila na kumtaka ofisa huyo kurudisha mizimu hiyo.

“Mimi ninachotaka ni watu wangu (mizimu) warudi kwa sababu hapa nilipo siwezi kufanya shughuli zozote za kichifu kwa sababu watu wangu hawapo” amesema Chifu huyo.

Chief Henel Mazengo amebainisha kuwa yeye ameshindwa kurejesha mizimu hiyo ambayo ni nyuki wa kizimu kwa sababu imekataa kurudi kwani nyumba yao imeharibiwa.

Ofisa huyo amejitetea kwa kusema alikuwa hajui kama mti huo ilikuwa unatumiwa kwa shughuli za kimila na ndiyomaana alitoa kibali cha mwananchi kukata mti huo kwaajili ya shughuli zake za ujenzi.

Aidha ameongeza kuwa yeye pia hawezi kuwarudisha nyuki hao hivyo ameomba waende kwenye vyombo vya sheria kwani tokea ameanza kazi hapo, hajawahi kuambiwa kuwa ule mti ni wakimila na mwenye jukumu la kusema ni chifu mwenyewe ambaye hakufanya hivyo.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Ardhi, Mali Asili, Utalii na Mipango
    miji..sit down pangeni mikakati ya kulinda hizi natural touristic attraction . Mti of this nature is unique .

    ReplyDelete

Top Post Ad