Rais Donald Trump Bana...Agoma Kabisa Kuvaa Barakoa "Kuvaa Barakoa ni Uchaguzi Binafsi wa Mtu"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Rais Donald Trump, ambaye siku zote amekuwa akipinga muongozo wa uvaaji barakoa uliotolewa na maafisa wa afya, amesema atavaa barakoa kama atakuwa ''katika mazingira ya watu yatakayomlazimu kufanya hivyo''.

Bwana Trump ambaye amekwepa kujitokeza mbele Umma akiwa amevaa barakoa, pia amekuwa akishikilia msimamo wake kuwa kufunika uso hakuhitaji kuwa suala la lazima katika kudhibiti kuenea kwa ugonjwa wa Covid-19.

Kauli yake aliyoitoa kwa Fox News imekuja siku moja baada ya kiongozi wa Republican kutoa wito kwa Bwana Trump kuvaa barakoa ili aoneshe mfano.

Majimbo kadhaa nchini Marekani yameshuhudia ongezeko la maambukizi na vifo siku za hivi karibuni.

Marekani sasa ina watu zaidi ya milioni 2.6 waliothibitishwa kuambukizwa virusi vya corona na vifo zaidi ya 127,000.

Rais amesema nini?
Akizungumza na kituo cha habari cha Fox Business Network siku ya Jumatano, Bwana Trump alisema : ''Ninaunga mkono barakoa.''

Alipoulizwa kama atavaa barakoa, rais alisema: ''Kama nitakuwa kwenye mazingira ambayo yatalazimu kufanya hivyo.''

Aliongeza kuwa watu wameshawahi kumuona akiwa amevaa barakoa hapo kabla.

Bwana Trump alisema ''hatakuwa na tatizo '' kuvaa barakoa mbele Umma akisema ''na ni kama anapenda'' anavyoonekana akiwa amevaa barakoa.

Lakini Rais amerejea tena msimamo wake kuwa hafikirii kuwa kufunika uso linahitaji kuwa suala la lazima nchini Marekani, kwa kuwa kuna ''maeneo mengi nchini humo ambayo watu hukaa kwenye umbali mkubwa''.

''Kama watu wanahisi vizuri kuhusu suala hilo wavae.''

Bwana Trump aliulizwa pia kama anaamini bado kuwa virusi vya corona siku moja ''vitatoweka''.

''Ninaamini'' alisema .Ndio hakika, Wakati wa sherehe zijazo za uhuru tarehe 3 mwezi Julai, watu watakaohudhuria wanaomuunga mkono hawatalazimika kuvaa barakoa wala kulazimishwa kutochangamana.

Kituo cha kudhibiti magonjwa (CDC) mwezi Aprili kilipowataka watu kuvaa barakoa au kujifunika na nguo wanapokuwa maeneo ya watu wengi ili kudhibiti kuenea kwa maambukizi, Bwana Trump aliwaambia wanahabari kuwa hatafuata kanuni hiyo.

''Sidhani kama nitafanya hivyo,'' alisema wakati huo.

''Kuvaa barakoa ninapowasalimia marais, mawaziri, maikteta, wafalme na malkia- kwa kweli sioni nikivaa.''

Lakini Trump amesisitiza mara kwa mara kuwa kuchagua kufuata muongozo wa wataalamu wa afya kuhusu barakoa ni suala la uamuzi binafsi.

Mwezi uliopita, aliliambia jarida la Wall Street kuwa baadhi ya watu huvaa barakoa kama jambo la kiasiasa dhidi yake.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad