Maji ya Kisima Yaua Mifugo Msibani, Waombolezaji 380 Wanusurika

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Waombolezaji takribani 380 wamenusurika kifo baada ya kugundua kutumia maji ya kisima yenye sumu kwa kupikia na kunywa mara baada ya mifugo wakiwemo ng’ombe 16 kufa papo hapo baada ya kunywa maji hayo.

Mifugo mingine iliyokufa kwa kunywa maji hayo ni punda, bata na paka. Tukio hilo limeripitiwa kutokea juzi katika kijiji cha Mkusa katika bonde la ziwa Rukwa wilaya ya Sumbawanga na kusababisha taharuki kwa waombolezaji waliokusanyika kwenye nyumba ya ya mfugaji Elias Juma.

Taarifa kutoa eneo la tukio zinaeleza kuwa kabla ya waombolezaji hao hawajaanza kuyatumia maji yaliyokuwa kwenye kisima cha Juma, wanyama walichotewa na walipoyanywa walikufa papohapo.

Kamanda wa polisi mkoa wa Rukwa, Justine Masejo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa watu wawili wamekamatwa na wanashikiliwa na jeshi la polisi wakituhumiwa kumwaga sumu katika kisima.

Mwanza: Jambazi aliyevamia benki auawa na polisi
Ameeleza kuwa wawili hao ni majirani wa mfuaji Juma ambapo walishtakiana mahakamani katika shauri la mgogoro wa aridhi.

“Maofisa polisi na mtaalamu wa afya walifika kijijini hapo na kufanya uchunguzi wa kitaalamu na kubaini kuwa mifugo hiyo ilikunywa maji yenye sumu ambayo haikuweza kufahamika mara moja ” Ameeleza kamanda Masejo.

Amethibitisha kuwa hakuna mtu yeyote aliyeripotiwa kupoteza maisha kutokana na tukio hilo, na kubainisha wanayama waliokufa ni ng’ombe wa kisasa 16, punda, bata pamoja na paka.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad