AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Uongozi wa klabu ya Yanga umesema kitendo cha utovu wa nidhamu kilichofanywa na mchezaji wao Bernard Morrison katika mchezo wa jana wa nusu fainali ya pili ya michuano ya Azam Sports Federation Cup waliolala kwa mabao 4-1 dhidi ya Simba watakichukulia hatua.
Morrison alifanyiwa mabadiliko dakika ya 68 akaondoka moja kwa moja na hakukaa kwenye benchi kama ilivyo kawaida akionekana kuwa na hasira kwa mabadiliko hayo jambo ambalo uongozi umelitafsiri kuwa ni utovu wa nidhamu.
Afisa Muhamasihaji wa klabu hiyo Antonio Nugaz amesema kila kitu kina utaratibu wake na hatua stahiki zitachukuliwa na zitawekwa wazi.
Kwa upande wa mashabiki wameonyesha kukerwa na mchezaji huo nakusema hata kufungwa kwao kumechangiwa Morriosn ambae alikuwa kama mtalii uwanjani.
Katika mchezo wa jana winga huyo raia wa Ghana alishindwa kuonyesha makeke yake kama ilivyokua katika mechi ya ligi kuu ambayo alifunga bao pekee na la ushindi dhidi ya Simba,huku wengi wakiamini kwamba huenda kwa sasa hayupo tayari kuitumikia klabu hiyo.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK